Category: Jamvi la Kiswahili

  • KIVUKIO CHA KIFO

    Na: Dorothy Waweru
    dorothywaweru161706@daystar.ac.ke

    Picha kwa hisani ya: The Star

    Ni afueni kwa wakenya wote na haswa familia yake Bi. Mariam Kighenda kwa kutolewa katika hindi la Victoria.

    Shughuli hii iliyochukua siku kumi na tatu, imezifanya nyoyo nyingi sasa kupata na utulivu. Aila ya Bi. Mariam sasa inauhuru wa kuzipumzisha mili ya wapenda wao ambao wamesumbuka usiku kucha. Japo bado uchungu upo, tunamwomba Mwenyezi Mungu aweze kuilaza roho zao pahala pema peponi.

    Hata hivyo, Shirika la Kenya Ferry limekabiliwa na mashtaka chungu nzima kufuatia ajali iliyotokea katika kivuko cha Likoni. Ajali hiyo ilihusisha kutumbukia kwa gari moja kwenye bahari hindi mnamo Septemba ishirini na tisa mida ya saa kumi na mbili. Gari hilo lilikuwa na abiria wawili, Bi. Mariam Kighenda na mwanawe Amanda Mutheu.

    Yasemekana wawili hawa walikuwa wametoka kuzuru shamba katika kaunti ya Kwale na walikuwa wakirejea nyumbani walipopatana na kifo chao.
    Matukio yaliyojiri baadaye yanaashiria utepetevu mkuu wa shirika la Kenya Ferry katika kutekeleza majukumu yao ya kuhakikisha usalama wa wasafiri.

    Baada ya ajali hiyo kutokea siku ya Jumatatu tarehe thelathini Septemba, Kenya Ferry kupitia mtandao wa kijamii wa twitter ilitangaza kuwa watahakikisha kuna meli nne katika kivukio cha Likoni.

    Wakenya kupitia mtandao huo walituma jumbe zilizosheheni kughadhabishwa kwa usemi wa Kenya Ferry kwani la muhimu lilikuwa kuomba msamaha kwa familia ya walioadhirika badala ya kuwaambia wananchi kuwa feri nne zitatutumika kuwasafirisha abiria hapo likoni.

    Ni jambo la kukereketa maini kugundua kwamba shirika la feri halina mikakati bomba inayowahakikishia abiria usalama wao hasa wakati kuna tukio kama hilo linalohatarisha maisha yao.

    Uchunguzi ambao unaendelea kufanywa umebaini kwamba shirika la feri la humu nchini halina wapiga mbizi ambao wanasafiri katika feri mchana na usiku bali wanawategemea wapiga mbizi katika shirika la Kenya Ports Authority na jeshi la baharini humu nchini.

    Uhai wa mama Amanda na mwanawe haungekatizwa ghafla iwapo shirika la Kenya Ferry lingekuwa na wapiga mbizi katika chombo hicho wakati wa mkasa huo. Wapiga mbizi wangelikuwepo wangefanya hima kuwaokoa abiria hawa punde tu gari lao lilipoanza kuzama.

    Msemaji wa serikali Col Rtd, Cyrus Oguna alipokuwa akitoa taarifa aliwaambia wanahabari kuwa gari lilichukua chini ya dakika moja unusu kuzama kwa hivyo kulikuwa na muda tosha wa kuwaokoa wasafiri hawa.

    Sababu za kucheleweshwa kwa kutolewa kwa miili ya walioaga ni kuwa kuna meli zinazopita baharini kupitia bandari ya Mombasa kufanya biashara ambayo inailetea kaunti ya Mombasa fedha nyingi. Tunaelewa kwamba tukikatiza usafiri wa meli baharini uchumi wa Mombasa utaadhirika pakubwa.

    Sababu ya pili ni giza kali ambayo imeshuhudiwa baharini hivyo wapiga mbizi wanatatizika sana. Tatu ni mawimbi makali yanayovuma baharini hivyo shughuli za uokoaji zinagonga mwamba wakati huo hadi mawimbi yatulie. Lakini ile sababu muhimu zaidi ni kuhakikisha kuwa usalama wa wapiga mbizi na wale wote wanaohusika katika shughuli za uokoaji unadumishwa,” haya yalikuwa maoni ya msemaji wa serikali Col Rtd.Cyrus Oguna.

    Shirika la Kenya Ferry limeshuhudia visa kama hivi vya ajali bali ni hatua chache sasa zimechukuliwa kuimarisha utendakazi wao. Wasafiri hawana uhakika wa usalama wao kwani janga kama hili linaweza kutokea bila usaidizi wowote. Ni bayana kuwa uwepo wa kuwa tayari kukabiliana na mikasa ya baharini ni jambo linalofaa kutiliwa mkazo.

    Feri zote zinafaa kuwa na vyombo vya kuhakikisha usalama wa wasafiri na magari pia. Sheria mpya zinafaa kubuniwa ili kuwe na mpangilio katika feri hizi. Hakuna mtu ambaye anafaa kupoteza maisha yake kupitia kisa cha kuhuzunisha kama hiki.

    Picha kwa hisani ya: citizentv.co.ke

  • UONGOZI UPYA KATIKA KLABU YA DAYSTAR COMPASSION AND CARE CENTER

    Na Gladys Sheila
    gladyshila52@gmail.com

    Picha kwa hisani ya: Joseph Gichari

    Josephndungo55@gmail.com

    Klabu ya Daystar Compassion and Care Center (DCCC) almarufu DC3 iliyoko katika chuo kikuu cha Daystar ilisherehekea uongozi upya. DC3, ni klabu ambayo imekuwepo tangu mwaka wa (2013) huku lengo lake kuu likiwa kufahamisha wanadaystar kuhusu maswala ya afya, kuwasaidia kisaikolojia wanafunzi, wahadhiri, wafanyakazi na jamii ya Daystar kwa ujumla. Klabu hii imekuwa chini ya uongozi wa Bi.Susan Botto ambaye ndiye mratibu wake.

    Siku hii ya ndovu kumla mwanawe, iliyoadhimishwa katika chapeli iliwaorodhesha viongozi wake wa mwaka wa 2019-2020 huku waliowatangulia wakiwakabidhi faili za utendakazi wao. Siku hiyo ya aina yake ilianzishwa kwa tenzi za kumsifu na kumuabudu Mungu, hafla iliyoongozwa na kwaya ya Imela katika chuo kikuu cha Daystar. Hali kadhalika, wanafunzi, wahadhiri na wafanyakazi chuoni Daystar walipokea pipi huku ikiwa kiishara kuwa wasiokwenye ndoa wajihifadhi mpaka wakati wa kufunga ndoa.

    Kilele cha hafla hii ni ufahamu dhabiti wa klabu hicho na wanajopo ambao walikuwa Bi. Emmah Nguli na Bwana Allan Ball ambao ni washauri wa maswala ya saikolojia.

    Matayarisho ya siku hii isitoshe hung’oa habta wiki ikianza huku mada kuu ikiwa kuwahamasisha wanadaystar kufahamu afya zao. DC3 hukakisha kuna vitengo mbalimbali ambavyo vyaweza kuwasaidia kutambua hali zao za kiafya ikiwa upimaji wa ongoezeko au upungufu wa sukari mwilini, uchunguzi wa saratani, kuangaliwa meno na upimaji wa ukimwi. Ukabidhishaji wa nyara kutoka kwa naibu wa msimamizi mkuu wa wanafunzi Bi. Irene Kimani.

    Waliotuzwa walikuwa:
    1. David Obong’o- Rais
    2. Gladys Sheila- Naibu wa Rais
    3. Wilbert Kiprop- Katibu
    4. Kevin Korir- Mweka Hazina
    5. Maureen Minus- Mkurungezi wa Halfa
    6. Chris Waweru- Msaidizi wa Vikundi vya Msaada

    Erick Spira, rais anayeshika timu hiyo mpya mkono, aliwapongeza waliomtangulia na kuwahamasisha wanafunzi kuridhika kwa kasoro wanazojua wanazo kwani zina manufaa maishani. Kwa kuwa chanzo cha jambo ni mwisho wa kingine, timu hiyo ilijumuika na kukata keki ya kusherehekea uongozi upya na uliopita katika ofisi zao za DCCC.

    Kweli sote kama wanafunzi, wahadhiri na wafanyakazi twawatakia viongozi hao kila la heri wanapoongoza wanadaystar.

  • KUNA NINI KATIKA BARABARA YA MAGADI?

    C21B84F3-9D5B-4371-BC87-FD7C59550353wangukanuri181152@daystar.ac.ke

    Na: Wangu Kanuri

    Ilikuwa vuta nikuvute katika barabara ya Magadi baina wanafunzi wa chuo kikuu cha Multimedia na polisi. Wanafunzi wa chuo kikuu hicho waliandamana na kufunga barabara hiyo kufuatia ajali iliyomlaza mmoja wao katika hospitali kuu ya Kenyatta huku akiwa katika hali mahututi. Kamanda wa Langata bwana Gregory Mutiso aliwarai wasafiri kutumia njia mbadala wanapowatuliza wanafunzi hao waliokuwa wamekabwa koo. Ajali katika barabara hiyo zinazotamatisha maisha ya wanafunzi katika chuo kikuu hicho si jambo geni ndio maana maandamano hayo yaliyoonyesha kughadhabishwa kwa wanafunzi na madereva.

    Kwa kutaka kuchukulia haki mikononi mwao kwa mwanafunzi huyo aliye katika mwaka wake wa kwanza na ambaye wiki jana aligongwa na yu katika hali mahututi, wanafunzi hao waliokerwa walistahimili vitoa machozi ambavyo maaskari waliwarushia nao wakiwarushia mawe. Mwanafunzi huyo aligongwa na matatu iliyokuwa ikiendeshwa kwa kasi mno hapo karibu na lango la chuo hicho kikuu. Isitoshe wanafunzi hao walilalamikia polisi kwa kuchelewa kushughulika baada ya mwanafunzi huyo kugongwa.

    Uchungu uliokuwa nyoyoni mwa wanafunzi hao ulidhibitisha kuwa walikuwa wamekerwa na ajali zinazofanyika katika barabara hiyo zinazotamatisha nyoyo za wenzao huku wakikumbuka kuwa mwaka wa 2016 walipoteza wanafunzi  wawili katika barabara iyo hiyo. Zaidi ya hayo, walilalamikia kuongezewa kwa nauli kwa matatu ya tume ya Ongataline na kunyanyaswa na waendeshaji wa magari hayo.

    Japo gari hiyo iliyomgonga mwanafunzi hiyo I katika kituo cha polisi, usakaji wa dereva huyo aliyemgonga mwanafunzi huyo bado waendelea. Hali kadhalika wanafunzi watatu walikamatwa katika maandamano hayo.

  • Umaskini tuuangamize au tuupunguze

    Untitled
    PHOTO COURTESY: ARON MTURI

    Ni wangapi wamekuwa wakipoteza wapendwa wao kila mwaka kwa majanga yasiyoeleweka? Tume­kuwa tukijaribu juu chini kutafuta suluhisho, huku tukiambiwa kuwa kuna madaktari ambao hukesha wakitafuta dawa za kati ya magonjwa makuu yanayoangamiza binadamu. Kufikia sasa, bado watu wanatamani kupata suluhisho la jinsi watakavyopata dawa za magonjwa sugu kama vile UKIMWI…lakini la kushangaza ni kuwa hata ugonjwa wa Malaria unaweza kuti­bika, lakini kila siku, takriban watoto ELFU TATU wanaangamia. Ninavyofikiria ni kuwa, tumekuwa watu wanaojishughulisha na mengi hadi tunasahau madogo ambayo tunaweza kuyaondoa kwa haraka.

    Katika Jamii, vijana wana mengi am­bayo wanaweza kuyafanya ili kushughulikia hili tatizo la umaskini, lakini tuseme ukweli, TUMEZEMBEA! Nilifurahishwa sana na jumbe niliyoipata kutoka kwa vijana kadhaa wa chuo kikuu cha Daystar ambayo ilikuwa hivi, “Tumekualika katika mkutano wa vijana, am­bapo tutakuwa tukiongea kuhusu jinsi sisi kama vijana tunaweza kuangamiza umaskini.”

    Singetaka kukuelezeeni jinsi nilivyofika mkutanoni…nilifika mapema, na si uongo, nilitabasamu tangu hadi mwisho. Mkutano wenyewe uliongozwa na Bwana mmoja, Dan Orero, kwa kusema kuwa angependa kila mtu atoe maoni yake. Kivumbi kikaanza! Kwanza, Bwana mmoja aliamka na kusema kuwa kul­ingana na utafiti wa wataalam, imesemekana kuwa si rahisi KUUANGAMIZA umaskini. Tunaloweza kufanya ni KUUPUNGUZA… Kimya! Orero naye hakusema kitu, aliandika tu.

    Zaidi ya hayo, aliuliza kama tunapaswa kui­lalamikia serikali kuhusu kiwango cha juhudi za kuupunguza umaskini. Hili lilimfanya Bwana mmoja kusema kuwa hatupaswi kuitupia seri­kali lawama, kwani haiwezi kufanya kazi bila kushirikiana na wananchi. Kisha, mwengine aliongeza kuwa tunazo rasilimali za kutosha na pia uwezo chungu nzima, ambao tumekuwa tukiupata tangu shule ya msingi, na kuna njia ambazo tunaweza kuzitumia ili kuupunguza umaskini katika jamii.

    Karen, mmoja kati ya wengi waliokuwepo alisema kuwa wazazi wana jukumu kubwa sana katika kuhakikisha kuwa watoto wao watakuwa katika mstari wa mbele katika vita vya kupun­guza umaskini. Ili wazo hili lilete maana, Wa­zazi wana jukumu la kuwaunga mkono watoto wao katika lolote wanalotaka kufanya maisha­ni. Aliongeza kuwa watu wengi wamepata sha­hada, na wamekaa miaka kadhaa bila kazi kwa­sababu walichokifanya chuo kikuu hakiendani kamwe, na kilichokuwepo myoyoni mwao.

    Hakuna aliyenifurahisha kama bwana mmoja, Gordon Odhiambo, aliyeongea kwa lugha ya kiingereza, “let us not come to school to GET JOBS, but to GIVE BACK TO THE COMMUNITY.” Ijapokuwa mimi si gwiji wa lugha ya kiingereza, nilimwelewa na kupasua kicheko. Watu walinishangaa kwa kudhani kuwa alikuwa ameongea upuzi mtupu, bali nilicheka kwani alikuwa ameigonga akili yan­gu kwa maneno ya busara ambayo nilikuwa nimeyatamani kwa muda mrefu.

    Singependa kukueleza mengi, natumai umenielewa, lakini nitakuacha na swali amba­lo wengi wamekuwa wakijiuliza. Je, unafikiri kuwa umaskini unaweza kuangamizwa kabisa, au kupunguzwa tu?

    By: Aron Mturi

    (aronmmtunji@daystar.ac.ke)