Category: Michezo

  • Tetesi Za Mbappe

    {Picha kwa hisani ya Sky News}

     

    Na Abdul Shaban

     

    Mshambuliaji Kylian Mbappe wiki jana Jumanne aliripotiwa kuwa na kikao maalumu na rais wa Paris Saint-Ger-main, Nasser Al-Khelaifi kujadili hatima yake.  Rais wa PSG Al-Khelaifi alikiri kushtushwa na uamuzi wa mshambuliaji huyo kwamba hawezi kubaki kwenye timu hiyo hadi 2025. Kutokana na hilo, PSG ilimpa Mbappe wiki mbili za kuamua kama anabaki Parc des Princes kwa maana ya kusaini mkataba mpya au la basi auzwe kwenye dirisha hili hili la uhamisho wa majira ya kiangazi.

    Hivyo, Mbappe na Al-Khelaifi walitarajia kukutana jana ana kwa ana ana kwa ajili ya mazungumzo na kuwekana wazi juu ya hatima ya kila upande klabuni hapo. . Kuna ripoti zilidai kwamba Mbappe atakwenda kuambiwa hadi kufikia Julai 31 atatakiwa aweke wazi msimamo wake kama atabaki PSG hadi 2025 au milango ifunguliwe ya kupokea ofa ya kupiga bei mwaka huu.

    Real Madrid bado wanapewa nafasi kubwa ya kunasa saini yake, lakini miamba hiyo ya Bernabeu inaelezwa kwamba haina pesa za kugharimia uhamisho wake baada ya kumtumia mkwanja mrefu kwenye dirisha hili kunasa huduma ya kiungo Jude Bellingham kutoka Borussia Dortmund. . Kutokana na hilo, timu za Ligi Kuu England zinaweza kuingia kwenye mchakato wa kunasa saini yake ikiwamo Manchester United, Arsenal na Liverpool ambazo zote zimeripotiwa kufuatilia kwa karibu mchakato huo.

  • Je, muda wa mshambuliaji wa Manchester United, Christiano Ronaldo, umekwisha Old Trafford?

    (Picha kwa hisani ya News18)

    Na Abdul Shaban

    Manchester United ilitangaza siku ya Alhamisi jioni kwamba Cristiano Ronaldo hatakuwa nao watakaposafiri kwa ndege kwenda Bangkok Ijumaa kwa ajili ya mechi ya kwanza ya Erik ten Hag akiwa meneja.

     

    Ronaldo ameruhusiwa kusalia Ureno, kwa ruhusa ya United, kushughulikia suala la kifamilia ambalo halijawekwa bayana.

     

    Mchezaji huyo nmwenye umri wa miaka 37 , ikumbukwe, alipoteza mtoto wa kiume mnamo Aprili, wakati mpenzi wake alipojifungua pacha, mmoja tu ndiye alyenusurika.

     

    Hakuna kiasi cha pesa au umaarufu unaoweza kumkinga mtu kutokana na aina hiyo ya kiwewe.

     

    Hata hivyo habari hizo zilijiri siku tano baada ya hamu ya Ronaldo kutaka kuondoka United msimu huu wa kiangazi kuwa hadharani.

     

    Na ingawa hatakuwepo, hiyo itakuwa simulizi ambayo itatawala wakati wote ambapo klabu hiyo itakuwa nchini Thailand, na kisha Australia, ambako watacheza mechi ya Jumanne dhidi ya wapinzani wao wa zamani Liverpool.

     

    Saa moja kabla ya Ronaldo kubainika kwamba hatokuwa katika safari ya kuelekea Thailand , chanzo kimoja kinachoifahamu BBC Sport kilisema kuwa hakukuwa na nafasi ya mchezaji huyo kuwa katika safari hiyo.

     

    Hatua hiyo ilijiri kutokana na imani kwamba Ronaldo lazima alikuwa na mpango wa kuondoka kwasababu , iwapo hataondoka , kile kilichojiri Wikendi kisingefanyika.

     

    Chanzo chengine cha United pia kiliunga mkono hoja hiyo. Wao pia walikubaliana kwamba sakata hiyo itakwisha wakati Ronaldo atakapoondoka katika klabu hiyo alioyowasili kwa mbwembwe za aina yake Agosti iliopita , baada ya kujiunga huku klabu ya Manchester City pia ikiwa na hamu ya kumsajili.

     

    Kwa upande wao Man United inasema kwamba Ronaldo haendi popote , wakidai kwamba ana mwaka mmoja katika kandarasi yake kuondoka kitu kinachomfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi katika ligi ya premia na kwamba wanatarajia kwamba ataheshimu kandarasi hiyo.

     

    Hata hivyo klabu inapaswa kusema hivyo ili kulinda mali zao. Wanajua kuwa katika soka ni mara chache wachezaji wanashikiliwa na mikataba yao ikiwa wamedhamiria kuondoka, hakika si wachezaji wa hadhi ya juu kama Ronaldo.

     

    Wakati mwingine msimamo huo unaendelea kwa wiki – kama Bayern Munich wanavyofanya sasa na mshambuliaji Robert Lewandowski – lakini kawaida makubaliano hufanywa na mchezaji anapata anachotaka.

     

    Katika hali hii, ajabu ni kwamba haitokani na dhamira ya Ronaldo ya kuendelea kucheza kwa kiwango cha juu zaidi, na kwamba hali ingeweza kufikia kilele mapema zaidi. Baada ya yote, ilikuwa dhahiri United haingeweza kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa kipindi kirefu kabla ya msimu kufikia kilele chake.

     

    Msisimko wa mechi za kujiandaa kwa msimu mpya

    United wamezoea masuala kama haya kutawala safari zao za mechi za kujiandaa kabla ya msimu mpya.

     

    Miaka mitatu iliyopita, katika ziara yao ya mwisho, kabla ya Covid kuwazuia ghafla, mzozo ulitawaliwa na iwapo Paul Pogba aliyechukizwa angerudi kutoka Marekani kwa wakati ili ndege ielekee Perth. Alifanya hivyo – lakini Romelu Lukaku alidhihirisha hadharani kutoridhika kwake kwa kujielekeza kwenye vikao vya mazoezi ya baiskeli ili apone jeraha ambalo lilipungua mara tu alipoondoka kwenda Inter Milan.

     

    Hiyo ilikuwa ziara ya kwanza ya Ole Gunnar Solskjaer kama meneja wa United. Licha ya kupata uzoefu huo kama mchezaji. Ten Hag anakaribia kugundua ushabiki wa klabu hiyo huko Mashariki mwanzoni – na jina lake kuu halitakuwepo ili kuondoa tahadhari hiyo.

     

    Badala yake, Ten Hag atakapokabiliana na vyombo vya habari – pengine Jumapili – kwa mara ya kwanza tangu lipozinduliwa Old Trafford, atakuwa na maswali mengi ambayo huenda asiwe na majibu – yaani ni lini au ikiwa Ronaldo ataanza kushiriki mazoezi pamoja na wachezaji wenzake.

     

    Je, Ronaldo ndiye suluhu au tatizo?
    Kuna mawazo mawili kuhusu uwepo wa Ronaldo United

    La kwanza ni kwamba alikuwa mmoja wa wachezaji wawili pekee – kipa David de Gea ndiye mwingine – kuibuka kutoka kwa msimu mbaya uliopita bila sifa zao kuingia doa . Alifunga mabao 24, ikiwa ni pamoja na hat-trick mbili, na, bila yeye, United ingekuwa katika hali mbaya zaidi kuliko ile waliyoishia.

    Lakini kuna simulizi nyingine, kwamba Ronaldo alikuwa mmoja ya sababu kuu zilizoifanya klabu kumaliza pale ilipomaliza.

    Inasemekana mara nyingi Ronaldo hapandi juu uwanjani – mkakati uliowekwa na mkufunzi Ralf Rangnick aloitarajia kutekeleza katika klabu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Solskjaer mnamo Novemba. Pia ndio mbinu ilioanzishwa na Ten Hag katika timu yake huko Ajax.

     

    Lakini je, uwepo wa Ronaldo ulikuwa mbaya pia?

    Alitofautiana na Harry Maguire kuhusu unahodha na, kwa kuzingatia hadhi ya Ronaldo, ni rahisi kufikiria angekuwa na maoni ya moja kwa moja kuhusu mambo mengine pia. Aliondoka uwanjani kwa kusuasua mara nyingi baada ya mechi, kwa hivyo anaweza kuwa anasema nini faraghani kutokana na hali mbaya ya jumla Old Trafford?

     

    Ni kweli Ronaldo akienda, United hawana nambari tisa – na hawajamtafuta.

     

    Lakini City wameshinda mataji mfululizo ya Ligi Kuu bila hata moja. Kiuhalisia, matarajio ya United ni ya chini sana na tayari wana idadi ya washambuliaji wa kimataifa wenye kasi ambao, labda, wanaweza kubadilishana. Kuwasili kwa Christian Eriksen kutaongeza ubunifu unaohitajika kwenye kikosi chao. Inatarajiwa kutakuwa na uimara zaidi katika safu ya kiungo hata kama harakati za kumtafuta Frenkie de Jong wa Barcelona zitashindwa kufanikiwa.

     

    Wiki chache zijazo zitakuwa muhimu kwa Hag Kumi.

     

    Anajua Ronaldo atakosekana mwanzoni mwa kipindi chake. Kwa uwezekano wote hatakuwepo kwa safari nzima.

     

    Jukumu la Ten Hag katikia eneo la mashariki na kwingineko ni kuandaa mpango ambao utafaa bila yeye. Msimu wa United unaweza kuutegemea.

  • ANGELLA OKUTOYI ASHINDA MASHINDANO YA WIMBLEDON

    (Picha kwa hisani ya The Standard)

    Na Gertrude Prosper

     

    Mchezaji wa tenisi, Angella Okutoyi mwenye umri wa miaka kumi na minane aibuka kuwa mwanamke wa kwanza kutoka Kenya kushinda mashindano ya Wimbledon. Katika mashindano hayo ya fainali, Angella alikuwa akishirikiana na Mholanzi Rose Marie Nijkamp katika timu ya wanawake Julai 9, 2022.

    Baada ya kushindwa katika seti ya kwanza ya 3-6 Okutoyi pamoja na mchezaji mwenzake waliamua kujikakamua na kushinda seti ya pili. Wapinzani hao, Kayla Cross na Victoria Mboko walishindwa (11-9) dhidi ya Nijikamp na Okutoyi (3-6, 6-4).

    Angella amevunja rekodi na kuwa Mkenya wa kwanza kufika katika fainali , akishirikiana na mwenzake Rose Marie, baada ya kuwashinda wapinzani wao Nikola Daubenova kutoka Serbia na Circa Bagaric kutoka Kroeshia (6-3 6-4) katika nusu finali.

  • TETESI ZA SOKA ULAYA

    Na Abdul Shaban

     

    Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo

    Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo, 37, ameafiki haja ya Manchester United ya kusaini mkataba na mshambuliaji mpya. (Express)

     

    Mshambuliaji wa Manchester City Mbrazil Gabriel Jesus

    Tottenham wana matumaini ya kuwapiku mahasimu wao wa kaskazini mwa London Arsenal katika mbio za kumsaka mshambuliaji wa Manchester City Mbrazili Gabriel Jesus kwa ofa ya soka ya Championi Ligi . (Mirror)

     

    Raheem Sterling

    Mshambuliaji wa Manchester City na England Raheem Sterling, 27, amekuwa akiwauliza watu kuhusu maisha katika magharibi mwa London huku klabu ya Chelsea ikiwa na nia naye. (Athletic)

     

    Dau la awali la £21.5m kwa ajili ya Sterling limekataliwa. (Fabrizio Romano)

     

    Chelsea wanaweza pia kumuhitaji mlinzi wa Manchester City mwenye umri wa miaka 27- Mholanz Nathan Ake. (Telegraph, subscription required)

     

    Mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Romelu Lukaku

    Mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Romelu Lukaku, 29, yuko tayari kurejea katika Inter Milan kwa gharama ya mkopo wa £8.5m pamoja na marupurupu aliyokubaliwabaina ya klabu hizo. (Mail)

     

    Manchester United wanaangalia uwezekano wa kufanya dai jipya kwa ajili ya kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi mwenye umri wa miaka 25 Frenkie de Jong. (Fabrizio Romano)

     

    Kiungo wa kati wa Wolves na Ureno Ruben Neves

    Kiungo wa kati wa Wolves na Ureno Ruben Neves, 25, yuko katika orordha ya Manchester United ya wachezaji inayoweza kusaini mkataba nao iwapo watashindwa kusaini mkataba na De Jong. (Fabrizio Romano, via givemesport)

     

    Newcastle wamepewa ofa ya fursa ya kusaini mkataba na mlinzi Mivory Coast Eric Bailly, 28, kutoka Manchester United. (Mirror)

     

    The Magpies pia wameambiwa kuwa ni lazima walipe £50m kusaini mkataba na winga wa Bayer Leverkusen na Ufaransa Moussa Diaby. (Sun)

     

    Meneja wa Uholanzi na meneja wa zamani wa Manchester United boss Louis van Gaal alihusika kwa sehemu katika kumzuwia mlinzi wa Ajax Mholanzi Jurrien Timber, 21, kuhamia Old Trafford. (Marcel van der Kraan, Sky Sports)

     

    Ajax wametenga euro milioni 40 (£34.3m) wanazotaka kuzitoza Sebastien Haller, huku Borussia Dortmund wakiwa na nia na mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27- kutoka Ivory Coast. (90min)

     

    Sunderland, Huddersfield na Bristol City wameweka dau la nyongeza la have £1m kwa ajili ya kiungo wa kati Muingereza mwenye umri wa miaka 21 anayechezea klabu ya AFC Wimbledon Jack Rudoni. (Sun)

  • PENYE SAMIA PANA SULUHU

    (Picha kwa hisani ya SportsArena)

    {Na Abdul Shaban}

     

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameonyesha nia ya kuomba kuandaa AFCON mwaka 2027 kama Tanzania itapata viwanja vingine vitatu vipya zaidi ya vilivyopo.

    Rais Samia aliyasema hayo wakati akipokea Kombe la Dunia 2022;

    “Kwa sasa tuna hiki cha Mkapa, Amaan Zanzibar, hivyo bado viwanja vitatu tuweze kujihakikishia kufanya maombi ya AFCON 2027 iletwe Tanzania,”

    Alisema Samia huku kampuni ya Coca Cola ikiahidi kujenga viwanja vingine vitatu, kimoja Dodoma na viwili Dar-es-salaam.