Category: Habari

  • MAKAMU CHANSELA WA CHUO KIKUU CHA DAYSTAR ATEULIWA KAMA MWAKILISHI WA KITAIFA WA BODI YA CHAMA CHA ELIMU YA MAREKEBISHO, MAREKANI.

    [Picha kwa hisani ya Prof. Laban Ayiro Facebook]

     

    Na Ashley Mbashu

     

    Makamu wa chansela, Profesa Laban Ayiro, ateuliwa kuwa mwakilishi wa bodi ya chama cha Elimu ya Marekebisho,  Marekani.

    Chama hiki kinahusu wataalamu wanaofanya kazi kwenye vitengo vya watu wazima na watoto kote nchini. Wao hutoa mafunzo muhimu na mitandao yenye manufaa ili kuwawezesha kuwasilisha maelekezo yenye ufanisi na yenye kuleta mabadiliko kwa wanafunzi wao.

    Shirika hili la kimataifa kiliundwa mnamo mwaka wa elfu moja mia kenda na thelathini. Shirika hili limeweza kuwahudumia watoa nidhamu na mashirika ya elimu ya mabadiliko kote duniani kwa miaka mingi.  Limeweza kutimiza haya yote kupitia uongozi, mwelekeo na huduma wanazotoza. Shirika hili limeibuka la kipekee kwenye utetezi wa kitaalam nchini Marekani.

     

    Kama mwakilishi wa kimataifa wa chama husika, Profesa Laban ana jukumu la kuhakikisha uhusiano mwema kati ya shirika husika na mashirika mengine ya kimataifa,  na taasisi zinazohusika na elimu ya marekebisho na nyanja zisizo za Marekani. Pia, atatakiwa kurahisisha mawasiliano kati ya shirika la kimataifa na washirika wao wa kimataifa.

     

    Profesa Ayiro pia atahitajika kuwakilisha muungano kwenye mikutano ya kimataifa na mingine ambapo pia atatakiwa kushiriki maarifa na kuzungumza kwa niaba ya wanachama wa shirika hilo.

     

    Kuteuliwa huku kwa Profesa Ayiro kwenye nafasi hii kunaonyesha anavyojizatiti kwenye kazi zake na pia uongozi. Ni heshima na fursa kuu kwetu, wanafunzi wa chuo kikuu cha Daystar, kwani tutaweza kujifunza na pia kufuata nyayo zake. Uteuzi huu ni ushahidi wa mafanikio yanayoweza kufanikishwa kupitia bidii za mchwa, kujitolea na cha muhimu, dua.

     

    Sisi kama wanachama wa gazeti la Involvement, tunampa mkono wa pongezi, Makamu chansela, Profesa Laban Ayiro.

     

    Kongole!

  • MAONYESHO YA NANENANE

    (Picha kwa hisani ya Tanzania Agricultural Development Bank)

     

    Na Gertrude Prosper

    Nane Nane ni likizo ya umma nchini Tanzania inayosheherekewa tarehe 8 Agosti, kila mwaka. Ni siku ya maonyesho ya kilimo ambapo wakulima wote nchini wanafanya maonyesho yao ya mazao, mifugo, dawa, na bidhaa katika kanda mbalimbali.

    Leo, Agosti 8 2022 ni kilele cha maonyesho ya nanenane ambapo viongozi pamoja na wananchi wanatembelea mabanda tofauti kujionea mbinu mbalimbali za kilimo bora, uvuvi na mifugo. Wajuzi, wajasiriamali na wataalamu wapo kuadhimisha siku hii kwa kuonyesha bidhaa zao na virutubisho mbalimabli vya mifugo mfano kuku, nyuki, nguruwe na ng’ombe. Wakulima pia wanauza bidhaa kama mashine, dawa, wanatoa elimu na bima ya mazao shambani.

    Siku hii ni muhimu kwasababu inawapa watu fursa ya kuonyesha teknolojia mpya na maendeleo katika kilimo, na kujua zaidi kuhusu uvuvi na ufugaji wa wanyama tofauti. Inawapa watu pia elimu, ujuzi na njia mbalimbali ya kufanya kilimo bora ili kupata mazao mengi ya chakula na biashara. Hii inaongeza vyakula nchini na mapato kwa kuuza nje katika nchi mbalimabli.

    Heri ya Sikukuu ya Nanenane

  • Sherehe ya Eid-ul-Adha 2022

    (Picha kwa hisani ya Hindustan Times)

    Na Getrude Prosper

    Mwaka huu wa 2022, nchi tofauti tofauti duniani zimesheherekea sikukuu ya Idd kwenye tarehe tofauti. Baadhi ya nchi zimesherehekea siku ya Jumamosi Julai 9 2022 na zingine zimesherehekea siku ya Jumapili Julai 10 2022. Zaidi ya hayo, Waziri wa Usalama wa ndani, Fred Matiang’i ametangaza kuwa Jumatatu, Julai 11 2022 kuwa siku ya mapumziko ya kuadhimisha sikukuu ya Idd-ul-Adha nchini Kenya.

    Idd-ul-Adha ni siku ya kuchinja na huadhimishwa siku ya 10 ya Mwezi wa Dhul-hijjah, mwezi ambao waislamu huenda kuhiji Makka, Saudi Arabia. Sherehe za mwaka huu nchini Kenya zimekua tofauti kidogo kutokana na hali ya uchumi iliyofanya gharama ya maisha kua juu. Baadhi ya wafanyabishara wanadai kua msimu huu wamepata hasara kubwa kwasababu ya kupungua kwa wateja. Kabla ya mabadiliko ya hali ya uchumi, siku za sherehe hua ni siku za wafanyabiashara kuuza zaidi kuliko siku zingine kutokana na misururu ya watu wanokuja sokoni kununua bidhaa mbambali ikiwemo nguo na vyakula.

    Mwaka huu hamna dalili zozote zile za sherehe kwenye baadhi ya maeneo kama awali kutokana na gharama ya maisha kupanda. Vitu vimepanda bei wanunuaji wamepungua.

  • WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA JAPAN, SHIZO ABE AFARIKI DUNIA.

    (Picha kwa hisani ya OneIndiaNews)

    Na Gertrude Prosper

     

    Waziri Mkuu wa zamani wa Japan, Shinzo Abe amefariki dunia baada ya kupigwa risasi akiwa katika kampeni za chama chake cha Liberal Democratic Party (LDP) kwenye uchaguzi wa wabunge katika mji wa Nara Magharibi mwa nchi hiyo.

    Abe amefariki dunia hospitalini baada ya kulazwa akiwa mahututi kufatiwa kupigwa risasi katika mashambulizi hayo. Katibu Mkuu wa nchi ya Japan, Hirokazu Matsuno pamoja na Waziri Mkuu Fumio Kishida wamesema hali ya Abe ilikuwa mbaya baada ya kupata shambulio la moyo.

    Mshambuliaji huyo ameshakamatwa na maafisa wa usalama na walinzi wa Abe muda mfupi baada ya shambulio hilo.

    Shinzo Abe ni kiongozi wa zamani wa Japan kutumikia nchi hio kwa muda mrefu zaidi kuliko mawaziri wakuu wengine wote nchini humo. Abe alizaliwa Septemba 21 1954 jijini Tokyo na alianza harakati za kisiasa 1993 alipoteuliwa kuwa mwakilishi wa baraza la juu la bunge kisha akateuliwa kuwa katibu mkuu wa baraza la mawaziri Septemba 2005 kabla ya kuja kuchukua nafasi ya urais wa chama chake cha Liberal Democratic Party (LDP) mwaka 2006. Abe anatoka kwenye familia ya kisiasa ambapo babu yake alikua Waziri wa nchi hio kwanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1960 na baba yake alikua katibu mkuu wa baraza la mawaziri la nchi hiyo, cheo ambacho kinaonekana ni cha pili kwa ukubwa zaidi nchi humo. Abe alikua Waziri mkuu wa Japan akiwa na miaka hamsini na miwili mwaka 2006, kiongozi wa kwanza kijana kuchukua nafasi hiyo. Muhula wake wa kwanza madakarakani uliubikwa na majanga kutokana na matatizo yake ya kiafya na kumfanya ajiuzulu. Alirejea tena serekalini na kutumikia wadhifa wa Waziri Mkuu katika nchi ya Japan kutoka mwezi Disemba mwaka 2012 hadi mwezi Septemba mwaka 2020.

    Abe atakumbukwa kwa sera yake ya kiuchumi akijaribu kufufua uchumi wa Japan uliokua umedorora. Atakumbukwa pia kwa kuongeza bajeti ya ulinzi na kubadili sera ya kijeshi ya Japan iliyodumu kwa miaka sabini. Alipambana pia kuboresha mahusiano yake na China.