Tag: athlete

  • MWANARIADHA ELIUD KIPCHOGE AMEWEKA REKODI DUNIANI

    Na Wangu Kanuri
    kanuriwangu@gmail.com

    Picha kwa hisani ya: Reuters

    Oktoba 12 mwaka wa 2019 ni siku ambayo daima itakuwa kumbukumbu kwani mwanariadha Eliud Kipchoge amevunja rekodi aliyokuwa amejiwekea ya kukimbia kwa kilomita arubaini na mbili kwa muda wa saa moja na dakika hamsini na tisa.

    Isitoshe jina lake limeandikwa katika kitabu cha rekodi cha dunia cha Guiness. Eliud aliyekuwa amejibidisha na kuamini kuwa ataweka historia duniani, aliwafanya wakenya wengi kujumuika kumtizama akivunja rekodi hii iliyofahamika kama INEOS 159.

    Rais Kenyatta aliwaongoza wakenya katika kumhimiza Kipchoge kulenga lengo lake huku naibu wake mheshimiwa Ruto na bibiye wakisafiri Vienna kumpa mkono anapokimbia.

    Kusudio kuu lake Kipchoge lilikuwa kuonyesha kuwa hakuna pingamizi lolote iwapo mtu anataka kuwa wa kwanza katika lolote. Isitoshe, alisisitiza kuwa hashindani na wengine bali anashindana na muda na kuweka historia katika dunia.

    Shindano hili liliokuwa likitizamwa moja kwa moja katika mitandao, limewafunza watu kuwa; shindano letu si dhidi ya marafiki, maadui ama wenzetu bali dhidi ya muda. Pili, mbio yetu yapaswa kuwa dhidi ya lengo tulizojiwekea na mwishowe mbio yetu ni katika tunayonuia kulenga.

    Eliud Kipchoge vilevile amesema kuwa alikuwa mwenye tumbo joto baada ya kupokea simu kadha wa kadha kutoka viongozi wakuu katika serikali ya Kenya ikiwemo rais Kenyatta. Hata hivyo, bado alishikilia msimamo wake dhidi ya kuweka rekodi ya wanariadha duniani.

    Akizungumza baada ya shindano hilo, Kipchoge amesema kuwa imemchukua mwanadamu miaka sitini na tano kuweka historia katika mbio za dunia kwa hivyo yeye amejazwa na furaha ghaya kuweza kuifufua historia hii. Mwenyekiti wa INEOS bwana Jim Ratcliffe alisema kuwa hakuamini vile Kipchoge alikimbia mtawalia mbio ya kwanza kwa muda wa chini ya saa moja.

    Picha kwa hisani ya: New York Post
  • SHUJAA WETU

    Na: Wangu Kanuri

    kanuriwangu@gmail.com

    TOA maelezo yako kuhusu mchezo wa raga

    Raga ni mchezo ambao unahitaji nguvu haswa kwenye misuli. Mchezo huu umegawanywa katika makundi mawili makuu; ya wachezaji saba na ya wachezaji kumi na tano. Kundi hili la wachezaji saba hujulikana vyema kama rugby 7s ilhali hilo la wachezaji kumi na tano hujulikana kama rugby 15s. Vikundi hivi ndivyo vimepewa kipaumbele nchini ila kuna vingine.

    TUELEZE kwa ufupi kukuhusu

    Slyvester Miheso, ni mwanafunzi wa shahada ya Udhibitishaji wa Rasilimali za Nchi katika chuo kikuu cha Daystar. Anapenda kusikiza muziki, kufanya mazoezi na kutizama filamu. Isitoshe, mimi ni mchezaji wa kawaida katika timu ya Falcons ambayo ni timu ya raga katika chuo kikuu cha Daystar.

    NINI kilikuchochea kuupenda mchezo huu wa raga?

    Nilipojiunga na shule ya upili ya Mtakatifu Inyasi ndipo ari yangu ya kupenda mchezo wa raga ilianza. Nilijiunga na timu ya raga nikiwa kidato cha kwanza japo shingo upande kwa kuogopa kuumizwa. Baada ya kujiunga na mchezo huo nilijua sheria na masharti zinazomkinga mtu wakati wa kumenyana na hofu yangu ikapungua.

    NI mchezaji yupi katika raga hukuvutia? Kwa nini?

    Mchezaji ninayemuenzi anachezea timu ya na Mwamba anafahamika kama Collins Injera. Mchezaji huyu ana bidii na anapenda kuwapa mwelekeo wachezaji chipukizi ili waweze kubobea kama yeye. Isitoshe, Collins amejivunia taji nyingi katika ligi za Uingereza kwa kufunga mabao mengi.

    MCHEZO HUU umekuvunia tija ipi?

    Mchezo huu umeniwezesha kufadhiliwa kimasomo katika ya shule ya upili na ya chuo kikuu. Hali kadhalika, nimejivunia taji la mchezaji bora na pia mchezaji aliyefunga mabao mengi upande wa Division 2. Nimeweza kuzuru nchi ya Uganda na Rwanda na miji ya Kisumu, Kakamega, Nairobi, Meru, Nanyuki na Nakuru.

    UNAWASHAURI vipi wachezaji chipukizi?

    Wasififishe talanta zao kwani ni zawadi kutoka Maulana. Pili, wafanye bidii wakati wa mazoezi huku wakiamini wao ni wachezaji bora kwani jambo huanzia kwa kukata shauri akilini. Tatu, wasikate tamaa hata wakishindwa kwani kufeli si kujaribu bali kutojaribu.

    FB_IMG_1569857000774

  • THE WOMAN BEHIND THE SPORT

    By: Valyne Laibuta

    Kalaine Kathambi is a student at Daystar University who embodies excellence. She is not only pursuing her degree in Marketing but she is also one of the most valued female players for the Daystar Hockey team. Outside school, she also plays for the Reiners Hockey Club.

    Her love for hockey began in high school when she was in form two and once she picked up that hockey stick, she has never looked back. She describes hockey as being “thrilling” and unlike other sports, hockey puts more emphasis on the skill and technique. Therefore, due to her zeal and hard work she has perfected her skills and technique on the hockey pitch, allowing her to be able to go against the boys without even breaking a sweat.

    For Kathambi, hockey is more than a hobby because it has provided her with the platform where she has been able to find herself and grow into the strong woman she is. She adds, “Hockey has become her outlet” when she has been experiencing a bad day and needs to release that negative energy. Unlike other players, she goes that extra mile such as going to train even on days that the team is not training, investing in the best hockey gear and going for a morning jog to ensure that she is at the top of her game.

    “As females, our voices are not heard,” she said, “During tournaments, 16 male teams are enrolled while only 8 female teams are enrolled”. This is one of the challenges she has faced as a female hockey player. It is saddening that female hockey players can put in the work but still not be valued as highly as men. Another challenge she has faced is the injuries she has sustained during training, matches, and tournaments. She jokingly describes the injuries she has sustained such as “having cut my lip by being hit by the ball”.

    “It was the last game I played in high school” describes Kathambi when asked about her most emotional match, “it was a goal that was meant to determine if we would make it for nationals and I could not score”. She adds that she hopes to redeem herself when she meets the goalkeeper from that last match in their upcoming match against Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology.

    Lastly, she concludes by urging the Ministry of Sports, culture and the Arts to invest more in hockey and encourage more high school hockey players to pursue hockey once joining universities. She hopes to see more and more people joining her to train with the Daystar Falcons.