Category: Sports

  • MCHUANO WA KUKATA NA SHOKA

    Na: Dorothy Waweru
    dorothywaweru161706@daystar.ac.ke

    Picha: Wachezaji wakijikakamua uwanjani

    Sikukuu ya Moi chuoni Daystar ilisherehekewa kwa mbwembwe, vifijo na nderemo kwani katika uga wa “Santiago Barna Betheli” kama unavyojulikana na wacheza kandanda wengi, mchuano mkubwa ulikuwa ukiendelea. Mchuano huo uliandaliwa na wanafunzi wacheza kandanda ikiwemo; Walter Nalwa, Nicholas Atulo Snr, Cedrick na Dadiseh Olwaga ambao walinuia kujiburudisha katika mchezo huo wa miguu.

    Mchuano huo ulijumuisha timu sita zikiwemo: Blueboys, Rawa, Buffoons, Bomboclats, DCF handball na Fimbu. Timu hizi zilimenyana vilivyo ili kushinda zawadi murwa ambayo ilikuwa ni mbuzi mzima. Timu za Buffoons na Rawa ndizo zilifungua uga huo ambao ulikuwa na utelezi kufuatia mvua kubwa iliyokuwa imenyesha usiku wote.

    Timu ya Buffoons ilijikakamua katika dakika za kwanza huku Caleb Msando akiifungia timu hiyo bao la kwanza naye Nicholas Atulo Snr akifunga bao lao la pili. Timu ya Rawa ilijikakamua katika kipindi cha lala salama ambapo John Lemaiyan aliifungia Rawa bao lao la kwanza. Kitengo hicho cha kwanza cha mchezo kilipotamatika, Buffoons walikuwa wamefunga mabao mawili kwa moja.

    Mashabiki wa timu ya Buffoons walijaa uwanjani wakiimba nyimbo za ushindi kwani timu hiyo ingemchinja mbuzi kama zawadi ya ufanisi wao iwapo wangewashinda wenzao kwenye semifinali. Baada ya dakika chache za mapumziko, timu ya DCF handball ilijitosa uwanjani kumenyana na wachezaji wa timu ya Fimbu. Uzoefu mkuu katika mpira wa mikono wa timu ya DCF handball ulionekana kuwapa mkono uwanjani. Hata hivyo baada ya dakika kumi na tano Wallace kutoka timu ya Fimbu alifunga bao la kwanza. Baada ya dakika zingine tano, DCF handball ilisawazisha kupitia mchezaji Ephantus.

    Baada ya nusu wakati wa mchezo huo, timu ya Fimbu ilifunga bao lingine ambalo liliwawezesha kuibuka washindi katika kitengo hicho kwa mabao mawili kwa moja. Timu ya Blueboys vilevile ilichuana na timu ya Rawa huku wakifunga bao lao la kwanza ambalo lilikuwa la pekee katika mchezo huo hivi basi kuibuka washindi dhidi ya Rawa.

    Hata ingawa jua lilikuwa mtikati, wachezaji wa Bomboclat waliingia ugani kumenyana na DCF handball. Yasemekana kuwa wachezaji wa Bomboclat walikuwa wamekesha wakijitayarisha kwa mchuano huo wa kipekee. Katika dakika za kwanza, Bomboclat ilifunga bao lao la kwanza na baadaye kufunga la pili. DCF handball ilijizolea nunge hivi basi Bomboclat kuibuka washindi.

    Isitoshe, kabla ya semi fainali, Bomboclat ilichuana na Fimbu na wakailaza Fimbu bao moja kwa nunge. Timu zilizofuzu kwenye semi fainali ni Fimbu, Buffoons, Bomboclat na Blueboys. Mechi ya kwanza katika semi fainali ilikuwa kati ya Buffoons na Fimbu. Buffoons walilazwa bao moja la kufunga virago baada ya kucheza kwa ukakamavu mwingi sana.

    Nyuso za wachezaji wa timu ya Buffoons zilijaa simanzi kwani mbuzi alikuwa amewakwepa. Lisilobudi hubidi, Buffoons walidondolewa kwenye mchuano wakabaki kuwa mashabiki tu. “Ni uchungu sana mama kubeba mimba tumboni kwa miezi tisa halafu anampoteza mwana wake. Nasikitika sana kuwa tumeshindwa,” Duncan Olile, kipa wa timu ya Buffoons alisema.

    Timu za Bomboclat na Blueboys zilichuana kwenye mchezo wa pili katika semi fainali huku Bomboclat ikiibuka mshindi baada ya kuilaza Blueboys mabao mawili kwa nunge. Washindi wa semi fainali walikuwa Bomboclat na Fimbu. Wakati ukiwa saa kumi na mbili kamili, mchuano kati ya timu hizi mbili ulianza huku Bomboclat ikifunga mabao mawili mida ya dakika za kumi na tano za kwanza. Japo Fimbu iling’ang’ana kiudi na uvumba kujizolea angalau bao moja, jitihada zao hazikuzaa matunda kwani katika kipindi cha pili cha mchezo huo, Bomboclat ilifunga bao lingine. Bomboclat wakafunga mabao matatu kwa nunge.

    Mbwembwe na shamrashamra zilijaa uwanjani wakati ambapo wachezaji wa Bomboclat walipokabidhiwa mbuzi wao. Wachezaji waliachwa ugani wakisherehekea ushindi wao huku mashabiki wakiungana nao kushangilia ushindi wao.

  • MWANARIADHA ELIUD KIPCHOGE AMEWEKA REKODI DUNIANI

    Na Wangu Kanuri
    kanuriwangu@gmail.com

    Picha kwa hisani ya: Reuters

    Oktoba 12 mwaka wa 2019 ni siku ambayo daima itakuwa kumbukumbu kwani mwanariadha Eliud Kipchoge amevunja rekodi aliyokuwa amejiwekea ya kukimbia kwa kilomita arubaini na mbili kwa muda wa saa moja na dakika hamsini na tisa.

    Isitoshe jina lake limeandikwa katika kitabu cha rekodi cha dunia cha Guiness. Eliud aliyekuwa amejibidisha na kuamini kuwa ataweka historia duniani, aliwafanya wakenya wengi kujumuika kumtizama akivunja rekodi hii iliyofahamika kama INEOS 159.

    Rais Kenyatta aliwaongoza wakenya katika kumhimiza Kipchoge kulenga lengo lake huku naibu wake mheshimiwa Ruto na bibiye wakisafiri Vienna kumpa mkono anapokimbia.

    Kusudio kuu lake Kipchoge lilikuwa kuonyesha kuwa hakuna pingamizi lolote iwapo mtu anataka kuwa wa kwanza katika lolote. Isitoshe, alisisitiza kuwa hashindani na wengine bali anashindana na muda na kuweka historia katika dunia.

    Shindano hili liliokuwa likitizamwa moja kwa moja katika mitandao, limewafunza watu kuwa; shindano letu si dhidi ya marafiki, maadui ama wenzetu bali dhidi ya muda. Pili, mbio yetu yapaswa kuwa dhidi ya lengo tulizojiwekea na mwishowe mbio yetu ni katika tunayonuia kulenga.

    Eliud Kipchoge vilevile amesema kuwa alikuwa mwenye tumbo joto baada ya kupokea simu kadha wa kadha kutoka viongozi wakuu katika serikali ya Kenya ikiwemo rais Kenyatta. Hata hivyo, bado alishikilia msimamo wake dhidi ya kuweka rekodi ya wanariadha duniani.

    Akizungumza baada ya shindano hilo, Kipchoge amesema kuwa imemchukua mwanadamu miaka sitini na tano kuweka historia katika mbio za dunia kwa hivyo yeye amejazwa na furaha ghaya kuweza kuifufua historia hii. Mwenyekiti wa INEOS bwana Jim Ratcliffe alisema kuwa hakuamini vile Kipchoge alikimbia mtawalia mbio ya kwanza kwa muda wa chini ya saa moja.

    Picha kwa hisani ya: New York Post
  • GOODBYE AND GOOD RIDDANCE?

    By: Sumaya Hussein

    husseinsumaya1@gmail.com

    The Closure of Sportpesa and Betin in Kenya

     

    The closure of SportPesa and Betin in Kenya announced on Saturday the 28th of September 2019. The shutdown of operations by these two giant betting companies was seen through an internal memo circulated to the staff. 

     

    The internal memo stated that staff from these two companies will be laid off their duties by the end of September 2019. The reason behind this was said to be the hostile environment provided by the Kenyan government which imposed a 20% tax on all wins, affecting their profitability. This came as a shocker for most Kenyans due to the impact these firms have brought to the country.

     

    Firstly, it is important to mention some of the positive things these companies have contributed to the economy of Kenya. Sportpesa and Betin were responsible for supporting local sports teams through sponsorships. These teams include the National team, Harambee Stars, which was supported in the recent Africa Cup Of Nations (AFCON) by Betin, Gor Mahia, AFC Leopards and the Kenya Premier League altogether. 

     

    It was mentioned by the Football Kenya Federation manager, Nick Mwendwa, that the companies had sponsored local football with up to Ksh 600 million. The departure of these companies leaves the teams stranded not to mention sources tell us that players from teams of Gor Mahia and AFC Leopards have not been paid in over 2 months. The Kenya Premier League are also left without a sponsor and have no funds to pay the referees.

     

    One of the people who were openly happy about the closure of the betting firms was MP Kanini Kega. He mentioned that the country should be careful about the type of investors it allows into the economy. He also said that the firms caused addiction and led youth into looking for riches and easy money through gambling instead of hard work. 

     

    Kenyans took to twitter to address this matter. Some were very bitter, saying how the government should provide jobs for youth and support to the local sports teams instead. However, some shared the same opinion with MP Kega about betting being a disease and Kenyans were better off without it. 

     

    Looking at things from a different perspective, Kenya is ranked the third-largest gambling market in Africa behind South Africa and Nigeria. A study conducted by Amani Mwadime showed that approximately 2 million people in Nairobi alone participate in online betting. It has become a full-time occupation for some people and those who work find themselves betting with their colleagues at tea break, lunch hour, evenings and during the nights. Moreover, students spend more time betting than they do with their academics. 

     

    Those who have experience in it know that one is likely to lose more than he/she will gain. The effects of losing itself are not very pretty. It makes youth go broke, fall into depression and even become suicidal. Furthermore, according to social anthropologists, it is among the list of things known to cause domestic violence. 

     

    As much as it has brought some good, betting also has its disadvantages which bring a strain to the growth and economy of a country. It is therefore actually safe to say goodbye and good riddance to Sportpesa and Betin. 

  • RESULTS FOR KUSA LEAGUE MATCHES

    By: Brenda Mogina

    Kenya University Sports Association (KUSA) tournaments took place on the 27th to 28th September in Nairobi, Kenya.

    Daystar ladies Volleyball Falcons were crowned champions of Aberdares Mbiriri Nyeri GSU, KDF volleyball tournament that took place over the weekend at the foothills of Mt Kenya.

    Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology (JKUAT) were the biggest winners in soccer women after putting two goals past Daystar Falcons who did not manage to net any goal.

    Daystar University Handball women and men teams saw off Gresta 08:10 and 19:19 respectively before Daystar’s falcon soccer ladies vs Gresta ended with a 1-1 draw.

    Gretsa Club were also on the receiving end when they alienated Daystar’s Netball team 46-16 in Netball Men.

    Daystar Basketball Women saw off Kiriri Women 61-9 in another highlight of the weekend.

    The following are results from KUSA league matches that happened over the weekend:

    Soccer

    Daystar Falcons (City) vs KCA. 1-1
    Daystar Falcons Athi Vs JKUAT 0 – 2
    Daystar Falcons soccer ladies 1-1 Gresta

    Handball

    Daystar vs Gretsa
    Men 19: 19
    Ladies 08: 10

    Hockey
    Daystar vs JKUAT (hockey men)2-2
    Daystar vs Kenyatta University (hockey ladies) 0-8

    Basketball
    Daystar (KUSA basketball men)vs Kenyatta University 19-88
    Daystar (NBA men) vs PBC 58-46
    Daystar Ladies vs Kiriri women 61-9.

    Netball

    Daystar Vs Gretsa 16-46

    Below are the fixtures for upcoming games.

    13.jpg

  • SHUJAA WETU

    Na: Wangu Kanuri

    kanuriwangu@gmail.com

    TOA maelezo yako kuhusu mchezo wa raga

    Raga ni mchezo ambao unahitaji nguvu haswa kwenye misuli. Mchezo huu umegawanywa katika makundi mawili makuu; ya wachezaji saba na ya wachezaji kumi na tano. Kundi hili la wachezaji saba hujulikana vyema kama rugby 7s ilhali hilo la wachezaji kumi na tano hujulikana kama rugby 15s. Vikundi hivi ndivyo vimepewa kipaumbele nchini ila kuna vingine.

    TUELEZE kwa ufupi kukuhusu

    Slyvester Miheso, ni mwanafunzi wa shahada ya Udhibitishaji wa Rasilimali za Nchi katika chuo kikuu cha Daystar. Anapenda kusikiza muziki, kufanya mazoezi na kutizama filamu. Isitoshe, mimi ni mchezaji wa kawaida katika timu ya Falcons ambayo ni timu ya raga katika chuo kikuu cha Daystar.

    NINI kilikuchochea kuupenda mchezo huu wa raga?

    Nilipojiunga na shule ya upili ya Mtakatifu Inyasi ndipo ari yangu ya kupenda mchezo wa raga ilianza. Nilijiunga na timu ya raga nikiwa kidato cha kwanza japo shingo upande kwa kuogopa kuumizwa. Baada ya kujiunga na mchezo huo nilijua sheria na masharti zinazomkinga mtu wakati wa kumenyana na hofu yangu ikapungua.

    NI mchezaji yupi katika raga hukuvutia? Kwa nini?

    Mchezaji ninayemuenzi anachezea timu ya na Mwamba anafahamika kama Collins Injera. Mchezaji huyu ana bidii na anapenda kuwapa mwelekeo wachezaji chipukizi ili waweze kubobea kama yeye. Isitoshe, Collins amejivunia taji nyingi katika ligi za Uingereza kwa kufunga mabao mengi.

    MCHEZO HUU umekuvunia tija ipi?

    Mchezo huu umeniwezesha kufadhiliwa kimasomo katika ya shule ya upili na ya chuo kikuu. Hali kadhalika, nimejivunia taji la mchezaji bora na pia mchezaji aliyefunga mabao mengi upande wa Division 2. Nimeweza kuzuru nchi ya Uganda na Rwanda na miji ya Kisumu, Kakamega, Nairobi, Meru, Nanyuki na Nakuru.

    UNAWASHAURI vipi wachezaji chipukizi?

    Wasififishe talanta zao kwani ni zawadi kutoka Maulana. Pili, wafanye bidii wakati wa mazoezi huku wakiamini wao ni wachezaji bora kwani jambo huanzia kwa kukata shauri akilini. Tatu, wasikate tamaa hata wakishindwa kwani kufeli si kujaribu bali kutojaribu.

    FB_IMG_1569857000774

  • BASKETBALL FLOODLIGHTS 2019

    Photos courtesy:Joseph Gichari

    Josephndungo55@gmail.com

    On Thursday, 26th September 2019, Daystar Uiversity, Athi River Campus, hosted the annual Basketball Floodlights competition.

    During the Basketball competition there were the following matches: Daystar University ladies team versus Cooperative University ladies team and Daystar University Mens team versus United States International University Mens team.

    There were other events also held during the floodlights competition such as Dunk fest, skills challenge, crowd free throw competition and half court competition.

    Find the photos from the competition attached below.IMG-20191001-WA0017IMG-20191001-WA0018IMG-20191001-WA0019IMG-20191001-WA0020IMG-20191001-WA0021IMG-20191001-WA0022

  • THE WOMAN BEHIND THE SPORT

    By: Valyne Laibuta

    Kalaine Kathambi is a student at Daystar University who embodies excellence. She is not only pursuing her degree in Marketing but she is also one of the most valued female players for the Daystar Hockey team. Outside school, she also plays for the Reiners Hockey Club.

    Her love for hockey began in high school when she was in form two and once she picked up that hockey stick, she has never looked back. She describes hockey as being “thrilling” and unlike other sports, hockey puts more emphasis on the skill and technique. Therefore, due to her zeal and hard work she has perfected her skills and technique on the hockey pitch, allowing her to be able to go against the boys without even breaking a sweat.

    For Kathambi, hockey is more than a hobby because it has provided her with the platform where she has been able to find herself and grow into the strong woman she is. She adds, “Hockey has become her outlet” when she has been experiencing a bad day and needs to release that negative energy. Unlike other players, she goes that extra mile such as going to train even on days that the team is not training, investing in the best hockey gear and going for a morning jog to ensure that she is at the top of her game.

    “As females, our voices are not heard,” she said, “During tournaments, 16 male teams are enrolled while only 8 female teams are enrolled”. This is one of the challenges she has faced as a female hockey player. It is saddening that female hockey players can put in the work but still not be valued as highly as men. Another challenge she has faced is the injuries she has sustained during training, matches, and tournaments. She jokingly describes the injuries she has sustained such as “having cut my lip by being hit by the ball”.

    “It was the last game I played in high school” describes Kathambi when asked about her most emotional match, “it was a goal that was meant to determine if we would make it for nationals and I could not score”. She adds that she hopes to redeem herself when she meets the goalkeeper from that last match in their upcoming match against Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology.

    Lastly, she concludes by urging the Ministry of Sports, culture and the Arts to invest more in hockey and encourage more high school hockey players to pursue hockey once joining universities. She hopes to see more and more people joining her to train with the Daystar Falcons.